-->

Gigy Apania Kuokoka

MUUZA sura kwenye video za Bongo Fleva ambaye pia ni mtangazaji wa Kituo cha Redio cha Choice FM, Gift Stanfod ‘Gigy Money’ hivi karibuni amefunguka kuwa, katika maisha yake, ipo siku ataachana na mambo yote yasiyompendaza Mungu kisha kumtumikia muumba wake.

Akipiga stori mbili tatu na Global Publishers, Gigy aliweka wazi kuwa, katika maisha ya mwanadamu, hasa kijana hukumbana na changamoto nyingi za kimaisha ambazo wakati mwingine humfanya kumkosea muumba wake, lakini inafikia hatua anaamua kuacha kila kitu na kufanya yanayompendeza Mungu.

“Unajua sometimes tunadondoka dhambini, lakini si kwa mapenzi yetu, binafsi ipo siku tu, nitaachana na mambo ya kidunia na kusimama kwa Mungu,” alisema Gigy asiyeishiwa vibwanga.

Chanzo;GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364