-->

Joh Makini Afungukia Ishu Yake na Mimi Mars

RAPA anayetamba na ngoma ya Mipaka, Joh Makini amepangua tetesi zilizosambaa katika mitandao mbalimbali zikimuhusisha kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mdogo wa Vanessa Mdee, Mimi Mars.

 

Joh Makini amesema anashangaa taarifa hizo na kufafanua hakuna ukweli wowote kwa sababu Mimi Mars kwake ni sawa na mdogo wake.

“A Big No, Mimi Mars ni kama mdogo wangu, kwanza sisi ni kama familia moja hiyo haiwezi kutokea kabisa,”anasema.

Joh Makini ni mmoja wa wasanii wachache ambao ishu za mahusiano yake yamekuwa ya siri sana hivyo uwepo wa tetesi hizo umewashtua baadhi ya mashabiki wake.

Mwanaspoti

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364