-->

Kufanya Collabo na Man Fongo ni Hadi 2020- TID

Msanii wa Bongo Fleva nchini TID amesema atakuwa tayari kufanya kazi na msanii maarufu wa Singeli nchini Man Fongo ifikapo mwaka 2010 na siyo kwa sasa.

tid32

TID ameyasema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa na EATV kila siku ya Ijumaa, na kuweka bayana kwamba kwa sasa ana mambo mengi na kzi nyingi za kufanya hivyo hataweza kufanya Colabo na msanii huyo.

“Nitakuwa tayari mwaka 2020 na siyo sasa pamoja na kwamba utakuwa mwaka wa uchaguzi lakini ndiyo kitakuwa kipindi kizuri cha kufanya hivyo lakini kwa sasa hivi sipo tayari nina kazi nyingi nazifanya” Amesema TID

TID ameklazimika kuyasema hayo kufuatia ujumbe mfupi wa mtazamaji wa EATV aliyetaka kujua kama TID atakuwa tayari kufanya Colabo na Man Fongo.

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364