-->

Kutoka na Mzee Siwezi-Shilole

Msanii wa muziki wa bongo fleva Shiloe alimaarufu kama Shishi Baby amefunguka na kuwataka wanaume ambao wanategemea wanawake kuvalishwa, kulishwa wabadilike na kuanza kufanya kazi ili wasitegemee tena wanawake kuendesha maisha yao.

Shilole

Shilole anasema wanaume ambao wanapenda kutunzwa na wanawake ni wanaume sanamu, maana wanaume makini hawawezi kutegemea kulelewa na wanawake.

Haya mambo hayatakiwi kuwepo, ndiyo maana unaona wanaume wengi saizi hawataki kufanya kazi yaani mimi nikulipie hotel, nikununulie nguo, sijui unataka nini mimi ninunue sasa wewe hapo utakuwa mwanaume au sanamu la mwanaume” alisema Shilole

Mbali na hilo Shilole aligusia suala la wanaume ambao yeye hawezi kutoka nao na kusema wanaume wazee yeye hawezi kutoka nao kimapenzi

“Sema dah kutembea na mzee inahitaji moyo kweli kweli, mimi kiukweli siwezi hili jambo” alisema Shilole

eatv.tv

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364