-->

Mama Yake Dogo Janja Afungukia Ndoa ya Dogo Janja na Irene Uwoya

Mama mzazi wa msanii Dogo Janja Bi. Zaituni Omari, amesema habari za mtoto wake kuoa ni za kweli na yeye kama mzazi alimpa baraka zote, vinginevyo asingeweza kuoa.

Mama yake Dogo Janja ameyasema hayo alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari na kusema kwamba yeye kama mzazi ameridhika kwani pia ametimiza matakwa ya dini.

“Alishawahi kuniambia kuwa anataka kuoa na mimi nikampa baraka zote, alivyokuwa tayari alinijulisha akaniambia kama kuna uwezekano niende isipokuwa kuna mambo yakaingilia kati, ila kwa vile Madee ni kama baba yake na ninamuamini sana nikawaruhusu waendelee, kila anachofanya hafanyi yeye kama yeye lazima kiko nyuma yangu, sio stori za kiki ni kweli kaoa na hawezi kuoa bila kuwasiliana na familia yake”, amesema mama yake Dogo Janja.

Kuhusu suala la tofauti ya umri kati yake na Irene Uwoya, mama yake Dogo Janja amesema kwamba suala la umri halijalishi sana isipokuwa kikubwa ni maelewano.

“Nimeridhika kwa sababu hata dini yetu ya Kiislam Mtume Mohamad alioa mwanamke mkubwa, kwa hiyo umri haujalishi, kikubwa na maelewano”, amesema Mama yake Dogo Janja.

Ijumaa ya wiki iliyopita kulianza kuonekana kwa picha mtandaoni zinazoonyesha Irene Uwoya na Dogo Janja

EATV.TV

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364