-->

Masanja: Sikukurupuka Kugombea Ubunge Ludewa, Ajipanga Kugombea Tena

Mchekeshaji Masanja Mkandamizaji amesema akukurupuka kuwania ubunge wa jimbo la Ludewa, mkoani Njombe kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) baada ya aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo Deogratius Filikunjombe kufariki kwa ajali.

MASANJA378

 

Akizungumza katika kipindi cha Uhondo cha EFM Alhamisi hii, Masanja alizungumzia kitu ambacho kilimkwamisha kupata didhaa ya kugombea ubunge kupitia chama hicho.

“Yaani maana ya kukurupuka ni kujituka upo sehemu ambayo haukupanga kuwepo, ila mimi ile yote ni mipango,” alisema Masanja.

“Kwa hiyo mimi niliamua kugombea lakini maandalizi yalikuwa madogo, kwa sababu kile kifo kilitokea kwa ghafla wakati huo nipo kwenye kampeni za mweshimiwa. Kwa hiyo baada ya kutokea tatizo hilo mimi nitarudi jimboni na kuchukua form lakini pia watu ambao walipiga kura ni wenyeviti wa kata, kwa sababu ulikuwa uchaguzi mdogo, sasa ile ngoma ingepigwa na raia sasa hivi ningekuwa bungeni. Lakini bado umri wangu unaruhusu miaka mitano ijayo nitagombea tena,” aliongeza Masanja.

 Bongo5

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364