-->

Mashabiki Wakerwa na Kauli Hii ya Zari, Wadai Amewakejeli Maskini

Labda ukweli unauma.. Kwamba wengi tunatamani sana maisha mazuri anayoishi Diamond na mchumba wake, Zari the Bosslady. Wapo wanaoishia kutamani na kumuomba Mungu nao waje kuwa na maisha hayo, wengine hushukuru na hufurahi tu kwa kile walichonacho ama tumeseme wameridhika na kidogo wanachopata.

12750132_252336151771158_2006726058_n

Lakini wapo ambao hushindwa kujizuia kupata wivu na kuwachukia tu watu wenye mafanikio – wa kuitwa haters. Hayo ni majaribu makubwa waliyonayo mastaa duniani. Lakini sio mara zote huvumilia matusi na kejeli wanazozipata kwenye mitandao ya kijamii.

Wakati Zari akiendelea kula raha Ulaya na mchumba wake Diamond, ameendelea kutupiwa vijembe na watu kuwa hawajali tena wanae watatu aliowaacha Afrika Kusini, kwamba kila siku kiguu na njia na Diamond. Hilo limemkera, na ameamua kulijibu.

10012578_537251566436724_941236644_n

Staa huyo amepost picha hiyo juu na tafsiri yake kwa maneno hayo ni:

Watoto wangu wameniuliza, kwanini kila mtu amechukia? Nimewaambia tuna vitu ambavyo hawana. Wakati mnachukua, mimi naenda mall, kumwaga fedha. Naweza, huwezi

Lakini pia aliweka caption isemayo: Baadhi yenu hamtaelewa hili lakini ni sawa. Ninawajibika kwa ninachoandika, na sio unavyokielewa.

4

Hilo limeonakana kuwakera wengi, wakiwemo mashabiki wake. Baadhi waliongea mambo mazito kiasi cha kumfanya awajibu pia.

New

Well, good news ni kubwa ex wake, Ivan, amewachukua wanae na kuwapeleka kwenye kisiwa cha maraha cha Ibiza kula pizaa! So waswahili wanasema hiyo ni ngoma drooo… Pesa inaongea!!

Chanzo: Bongo5

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364