-->

Mr Blue Afunguka Kuanzisha Ubishoo Kwenye Bongo Fleva

Mkali wa wimbo ‘Mboga Saba’ Mr Blue amesema yeye ana mchango mkubwa katika mabadiliko ya muziki wa bongofleva nchini.

mr blu833

Mr Blue

Akiongea katika kipindi cha Ndoto Kubwa cha Clouds TV Jumapili hii, Mr Blue amesema yeye ndiye msanii wa kwanza kufanya muziki akiwa na swagga.

“Mimi baada ya kuingia kwenye muziki kuna vitu ambavyo nilivifanya mimi kama mimi ili kuonyesha utofauti, kuanzia kwenye kuvaa, swagga za kuimba, kutoboa masikio. Kwa hiyo hivyo vyote kwa wakati ule watu walikuwa wananiona huyu jamaa vipi, kumbe mimi tayari nilikuwa nimeshaiona future, ndio maana wasanii wengi waofanya muziki kwa swagga, utasikia ana flow kama Mr Blue, tayari tulishaacha alama huko ndiyo maana tunaendelea kufanishwa,”

Katika hatua nyingine Blue amesema yeye alikuwa anapenda kusoma kuliko kufanya muziki, lakini akaamua kujifunza kufanya muziki mpaka akaweza.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364