-->

Mtoto wa Ray, Jaden Afuata Nyayo za Tiffah wa Diamond

Tiffah ni mtoto maarufu zaidi kwenye mtandao wa Instagram Afrika akiwa na followers zaidi ya milioni moja. Mdogo wake, Nillan naye anafuata nyayo zake akiwa na followers zaidi ya 99k sasa. Akaunti zao husimamiwa na mama yao, Zari na hutumia Kimombo.

Na sasa mtoto mwingine wa mastaa wa Bongo, Jaden naye amejiunga kwenye kundi la watoto wa aina hiyo.

Jaden ni mtoto wa Ray Kigosi na Chuchu Hans aliyezaliwa wiki hii na tayari amefunguliwa akaunti kwenye mtandao huo. Yake inasimamiwa na mama yake na kama Tiffah na Nillan, amewafollow wazazi wake tu.

Katika kufurahia zawadi ya mtoto, Ray ameendelea kuweka wazi furaha yake kwa kuandika: Nikikuangalia Mwanangu Jaden Nakuwa Na Furaha Isiyo Kifani Na Kunipa Nguvu Ya Kupambana Na Maisha Ili Uishi Vizuri.. Mtoto ana Raha Yake Jamani asikwambie mtu Nyie Puyangeni Tu.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364