-->

Nora Afungukia Wasanii Kujiuza

MKONGWE katika fi lamu Bongo, Nuru Nassoro ‘Nora’ ambaye kwa sasa anajishughulisha na ujasiriamali baada ya soko kwenda halijojo, amedai biashara ya kujiuza inayofanywa na baadhi ya mastaa wa tasnia hiyo hailipi na itawaathiri zaidi baadaye.

Nora Katika Pozi

 

Akipiga stori na Za Motomoto News, Nora alisema ni vyema wakatafuta shughuli halali ya kufanya ili kujipa heshima na hadhi ya majina yao kuliko kuishi kwa kujiuza kwani wanadharaulika na kusemwa vibaya na wanaume wanaowachukua.

“Nafanya biashara ndogondogo za kuuza nguo za watoto na saluni hivyo nawasihi wasanii wenzangu wa kike waachane na biashara ya kuuza miili yao, kwani ni hatari na ina madhara makubwa,” alisema msanii huyo wa siku nyingi.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364