-->

Nyumba Mbili za Wastara Kupitiwa na Bomoa Bomoa

wastara45

Muigizaji wa filamu, Wastara Juma amejikuta katika wakati mgumu tena baada ya nyumba zake mbili kupitishiwa X kwaajili ya kubomolewa siku zijazo.

Katika ukurasa wake wake wa Facebook, Wastara ameandika:

Mashabiki wangu mwaka umeanza vibaya kwangu nyumba zangu mbili zimewekwa X na zitabomolewa siku yoyote kuanzia leo,siko sawa kabisa niombeeni dua presha imepanda,nawapenda sana

Akiongea na Bongo5, ndugu wa Wastara amethibisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa hali ya muigizaji huyo si nzuri kutokana na mshtuko alioupata.

“Kweli Wastara hali yake sio nzuri amepata mshtuko baada ya watu wa mazingira kuweka X katika nyumba zake mbili,” alisema dada huyo aliyejitambulisha kwa jina la Mariam uku akidai Wastara hawezi kuongea na simu.

 Bongo5

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364