-->

Ray C: Namtamani Ray Vanny

Msanii wa muziki wa bongo fleva Ray C amefunguka na kusema anamtamani sana msanii kutoka katika label ya WCB Wasafi Ray Vanny na amekuwa akipenda sana kazi zake na kuzisikiliza, hivyo anatamani kufanya naye kazi hata moja tu.

Ray C alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema anasikia Ray Vanny anaandikia wasanii wengi sana nyimbo hivyo na yeye anatamani kufanya naye kazi kutokana na uwezo wake wa hali ya juu.

“Nampenda sana yule mtoto Ray Vanny, anaadika sana mashairi, nasikia anaandikia wasanii wengi nyimbo hata mimi natamani kufanya naye kazi” alisema Ray C 

Mbali na hilo Ray C alimzungumzia Diamond Platnumz kama msanii ambaye amefanya mapinduzi sana na kuupeleka muziki wetu wa bongo fleva mbali zaidi

“Kiukweli mimi nam respect sana Diamond Platnumz amefanya jambo kubwa katika muziki wetu, kama hutaki kuelewa basi tu hutaki kuelewa, japo sisi tulikuwa tunasikika sijui Kenya wapi lakini dogo amepita sehemu zingine ambazo sisi hatukufika, ambaye haelewi mchango wa Diamond katika muziki huu sijui hata ana maana gani” alihoji Ray C  

eatv.tv

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364