-->

Scene za Mapenzi Zamtesa Mwanaheri

MWIGIZAJI wa Bongo Muvi, Mwanaheri Ahmed, amefunguka kuwa, suala la kucheza ‘sini’ (scene) za kimapenzi kwenye filamu huwa linamtesa hasa linapokuja suala la kumlaghai mwanaume.

Mwanaheri Ahmed

Akipiga stori na Showbiz Xtra , Mwanaheri alisema kuwa, pamoja na mwigizaji kupaswa kuvaa uhusika wa scene yoyote ile unayopangiwa, lakini kwake uhusika wa mapenzi huwa unamtesa na kumnyima usingizi.

“Scene za malavidavi kwangu huwa ni mtihani na sizipendi, huwa zinaninyima amani hasa ninapotakiwa kumlaghai mwanaume, wakati mwingine nahisi nikijibebisha sana, naweza kumkwaza baby wangu. Ila uhusika wa kukasirika hata kama utanikurupusha usingizini, nitakuwa huru nao,” alisema.

Chanzo:GPL

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364