-->

Shamsa Achekelea Mpenzi Mpya

STAA wa filamu Bongo, Shamsa Ford ameonesha furaha yake ya kuumaliza mwaka kwa kumpata mpenzi mpya, ambaye hata hivyo, alikataa kutaja jina lake.

Shamsa Ford

Shamsa Ford Akiwa Kwenye Pozi

Akizungumza na gazeti hili juzikati, Shamsa alisema mwaka huu pia umeweka historia kwa yeye kuweza kutimiza mambo yote aliyojipangia tangu alipoachana na baba wa mtoto wake.
“Nafurahi sana namaliza mwaka nikiwa nimetimiza malengo pia kuwa na mpenzi mpya ambaye ni mume wangu mtarajiwa, ndani ya mwaka huu nimejifunza siyo vizuri kuweka uhusiano wazi hasa kwenye mitandao ya kijamii, maana unajidhalilisha unaweza kujikuta leo uko na huyu kesho na huyu inakuwa ni aibu,” alisema Shamsa.

Chanzo:GPL

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364