-->

Siri ya Wema Sepetu Kupukutika Yafichuka!

VYUMA vimekaza? Siri ya staa mkali wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu kupukutika imefichuka baada ya picha zake kusambaa zikimuonesha akiwa hana lile shepu aliloliimba Dogo Aslay.

Kufuatia ishu hiyo, mashabiki wa Wema walipigwa na butwaa jinsi mwili wake huo ulivyopukutika. Ili kumaliza ubishi huo, Ijumaa Wikienda lilizungumza na Wema na kumuuliza kulikoni kupukutika mwili ambapo alisema kuwa, huko nyuma alikuwa hapendi kabisa kujihusisha na mambo ya kwenye ‘gym’ kwani alikuwa akiona hawezi kufanya hivyo kwa ajili ya kupunguza mwili, lakini siku zinavyozidi kusonga aliona ni bora kufanya hivyo kwa sababu mwili wake uliongezeka kupita kiasi.

“Unajua nilikuwa nikiangalia kila nguo ninayovaa inanibana. Wakati mwingine ni kubwa kabisa, lakini inakuwa hainitoshi, nikaona nina kila sababu ya kupunguza huu mwili ambao siyo mzuri hata kiafya,” alisema Wema.

Wema ambaye wikiendi iliyopita alikuwa nchini Rwanda kwa ajili ya Shoo ya Instagram Party alisema kuwa, sasa hivi anafanya mazoezi takriban mwezi mmoja, lakini ameanza kuona matunda yake na anajilaumu alikuwa wapi kwa kipindi chote hicho na kushindwa kufanya mazoezi kwani mwili aliokuwa nao usingekuwepo. “Nina mwezi mmoja sasa tangu nianze mazoezi ya kupunguza mwili, lakini ninafurahia maisha haya na najuta kwa nini sikuanza mapema,” alisema Wema.

Chanzo:GPL

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364