-->

Sugu Kuja na Shindano la‘Freedom’, Msindi Kupewa Milioni Tano

Baada ya wimbo wa ‘Freedom’ kufanya vizuri kwenye media mbalimbali, Sugu anajipanga kuandaa shindano litakaloshindanisha wimbo utakaouzidi wimbo huo.

sugu mbunge

Siku kadhaa zilizopita baada ya Sugu kuachia video ya wimbo wa ‘Freedom’ ulizua taharuki baada Mr Blue kulalamika kuwa Sugu kamuibia wimbo wake kabla ya uongozi wa studio ya MJ Record ambapo wimbo huo ulitayarishwa kuliweka sawa tatizo hilo.

Akizungumza kwenye kipindi cha FNL, kinachoruka kupitia EATV, Sugu amesema ‘tutaandaa shindalo la kushindanisha nyimbo itakayoizidi wimbo wa ‘Freedom’.

“Tumeshaongea na media moja ambayo tutapeleka wimbo wa ‘Freedom’ ambao wasanii wanaotaka watarekodi wimbo wataupeleka hapo. Kutakuwa na majaji kwenye shindano hilo watakaochagua nyimbo kumi bora na baadaye kupata nyimbo moja. Mshindi kwenye shindano hilo atapata shilingi milioni tano,” aliongezea.

Sugu amesema kwenye shindano hilo halitabagua msanii yeyote kila mtu anaruhusiwa hata awe Mr Blue.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364