-->

Wamehamia kwa Kajala na Shetta

UBUYU wa leo unawahusu mastaa wawili Kajala Masanja na Shetta kudaiwa kuwa ni wapenzi huku ikielezwa wanatumia mbinu ya danganya toto kwa kitendo cha Shetta kuonyesha ukaribu kwa mtoto wa Kajala anayeitwa Paula.

Kajala Masanja

Ziliwahi kuzagaa habari kuwa Shetta na Paula ni wapenzi lakini Shetta alipinga taarifa hizo na kusema kuwa anampenda mke wake na hawezi kumsaliti tena kwa mtoto mdogo kama Paula wa Kajala.

Hata hivyo, kwa sasa habari zimegeuka na madai mapya ya kudai Shetta ni mpenzi wa kajala na wanafanya siri kwa kulinda ndoa ya shetta.

Shetta

Mwanaspoti liliongea na Kajala na kusema, Shetta ni mshikaji wake na kwamba watu wametoka kuzusha kwa mwanae na sasa wameamua kumvaa yeye.

“Kweli huu Ubuyu wa Shetta unazunguka tu katika familia yangu, watu washahama kwa mwanangu wamehamia kwangu duu, sio kweli bana Shetta ni mshikaji wangu sana,” alisema Kajala.

Mwanaspoti

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364