Artists News in Tanzania

Mwanaher: Nipo Vizuri Kila Idara Mwanaher, Wengi Wamfananisha na Riyama

MTAYARISHAJI na mwigizaji wa kike Mwanaher Afcely anayefanishwa na mwigizaji wa kike Swahilihood Riyama ametamba kwa kusema kuwa hajivunii kufanana na Riyama bali ni uwezo wake katika uigizaji kwani anafanya vizuri na hata wengine wanashindwa kumtofautisha na Riyama kwa kuigiza kwa ufasaha.

“Nipo kikazi zaidi na unajua kama unafananishwa na msanii mwenye uwezo mkubwa ni kama vile unadaiwa na wapenzi wa filamu hakuna asiyemjua pacha wangu Riyama kwa kuwa na uwezo mkubwa katika filamu na sijamwangusha,”anasema Mwanaheri.

Mwanadada huyo mwenye stashahada ya manunuzi anasema kuwa alikuwa anaigiza filamu kutoka kwa watu hadi alipotengeneza filamu yake ya Pumu na kuwashirikisha wasanii wengine wa filamu Bongo, kwake anahisi ana deni kubwa kufananishwa na mkongwe na anashukru kwa msaada anaopewa na Riyama.

FC

Comments

comments

Exit mobile version