Artists News in Tanzania

Bwana Misosi Amwimbia Rais Magufuli

BAADA ya kimya cha muda mrefu katika muziki, msanii Joseph Lushalu ‘Bwana Misosi’, ameamua kurudi kwa nguvu na wimbo wa kumsifia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli.

Wimbo huo unaoitwa ‘Makofi kwa Magufuli’, umeimbwa chini ya ushirikiano kati yake na msanii Nuruel.

“Nimekuja na ujio mpya wa funga mwaka kwa ajili ya kumshukuru Rais wetu kwa kazi yake anayoifanya tangu kuchaguliwa kwake,” alisema Bwana Misosi.

 

Comments

comments

Exit mobile version