Artists News in Tanzania

Ray: Nilishawahi Kumuokoa Nay wa Mitego Asipigwe

STAA wa Bongo Movie, Vincent Kigosi ‘Ray’ kwa mara nyingine ameendelea kuteka ‘headlines’ baada ya kuibuka na kudai kuwa alishawahi kumuokoa staa wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego asipigwe.

Akizungumza asubuhi hii katika kipindi cha Leo Tena kinachorusha na Clouds FM, Ray alisema kuwa alipokuwa katika shoo ya Fiesta Mwanza, Nay alivamiwa na kundi la wasanii wa Bongo Movie na kutaka kupigwa.

“Nilifanikiwa kumzuia kwasababu wasanii walikuwa wengi wakiongozwa na Wema Sepetu sasa nashangaa mwenzangu Nay ananisakama natumia pesa zote za mauzo ya filamu namalizia kwenye mkorogo,” alisema Nay.

Chanzo:GPL

Comments

comments

Exit mobile version