Artists News in Tanzania

Vita Kali ya Maneno Mtandaoni Kati ya Zari ‘Mama Tiffah’ na Wema Sepetu

zarivs wema

Ni muendelezo wa vita ya maneno isiyoisha kati ya anayejiita Zari The Bosslady na wa kuitwa Tanzanians sweetheart Wema Sepetu.

Vita hiyo imeendelea leo kwa Zari kuanza kumtupia mafumbo mwenzie Wema,wapambe wa Wema wakacharuka na kumuita boss wao Wema ambaye alitaharuki na kuuliza kipi kinachoendelea?
Ndipo mpambe wake anayejiita wemareplies alipomuwekea screen shot ya aliyoyasema Zari.
Wema nae akajibu huku akisisitiza hana muda na Zari wala kaka (Diamond)

Kama haitoshi akapost picha huku akiweka caption ya kuwa kafunzwa na mamie kugombana na watu wazima (Zari) ni kukosa adabu.

Ndipo Zari nae akamjibu kuwa yuko busy na kazi,asijisumbue.

Credit : Nifah on JF

Comments

comments

Exit mobile version