Artists News in Tanzania

Malaika: Nimechoka Kufananishwa na Lulu

MSANII wa Muziki wa Kizazi Kipya anayefanya vizuri, Malaika Exavery amesema anakerwa na kitendo cha watu wengi kumfananisha na muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’.

Akizungumza na gazeti hili, Malaika alisema huko nyuma alipokuwa akifananishwa na msanii huyo hakujali, lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda imekuwa ni shida hadi wengine wanamsimamisha.

“Unajua kufananishwa na mtu siyo tatizo, lakini kwa hali ilivyo hivi sasa lazima mtu usikie kuchoka kabisa kwa sababu hata wakati mwingine unaendesha gari mtu anakusi mamisha halafu akikuangalia usoni vizuri anaondoka, anasema alidhani ni Lulu,” alisema Malaika.

Chanzo: GPL

 

Comments

comments

Exit mobile version