-->

Amini: Linah Amepoteza Uhalisia Wake wa Mwanzo Kiuimbaji

Amini aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Linah uliodumu kwa miaka mingi kabla ya kuachana na kila mmoja akawa na maisha yake.

linnah45

Pia Amini aliwahi kumwandikia msanii huyo nyimbo kadhaa zilizofanya vizuri. Lakini sasa hitmaker huyo wa ‘Bado Robo Saa’ amesema kuwa Linah wa sasa si yule wa zamani katika uimbaji.

“Linah wa sasa anakosa uyeye aliokuwa nao mwanzo wakati mimi namuandikia nyimbo,” Amini alimwambia mtangazaji wa Kings FM, Prince Ramalove.

“So nyimbo anazozipata sasa hivi sio nyimbo za kuimba yeye. Nafikiri pia mwandishi anayemuandikia bado hajamjulia jinsi ya kumwandikia nyimbo za aina gani au idea ya aina gani, vile vile studio anazorekodia au producer anayerekodi naye anakuwa hajamjulia,” aliongeza.

Amini anasema bado ana uwezo wa kumwandikia Linah kwakuwa ni kwake ni sehemu ya biashara.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364