-->

Lulu Diva, Amber Lulu Hakuna Bifu

Muuza sura kwenye video za Kibongo, Lulu Abass ‘Lulu Diva’ (pichani juu) na mwenzake Amber Lulu (pichani chini) hawana bifu lolote isipokuwa kuna watu wana mpango wa kuwagom-banisha.

lulu_diva

Akichonga na Risasi Vibes, Lulu Diva alifunguka kuwa awali aliposikia kuwa Amber alimpaka matope kwenye ‘interview’ aliyofanya na redio fulani Bongo, alipaniki na kumtafuta ili amueleze kulikoni, lakini Amber alimwambia hakuna kitu kama hicho na kumtaka kuchunguza mwenyewe.

“Nilichunguza na kukuta kumbe si kweli, niligundua ni watu wasiopenda ushoga wetu ndiyo walikuwa wanajaribu kutukosanisha na si vinginevyo,” alisema Lulu Diva.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364