Vanessa Mdee Amjibu Afande Sele
Msanii Vanessa Mdee ameshindwa kuvumilia kukaa kimya baada Rapa Afande Sele kusema kuwa Said Karoli ana uwezo mkubwa kisanii kuliko Vanessa Mdee
Vanessa Mdee ameonyesha kutofurahishwa na kauli ya Afande Sele na kusema alikuwa anamuheshimu na kumtambua msanii huyo kutokana na heshima yake kwenye muziki huu lakini amechoshwa, kuzunguziwa na mtu huyo katika vitu visivyoeleweka
“Siwezi kujibishana na wewe itakuwa utovu wa nidhamu baba. Ila inasikitisha kwamba mtu ninayemheshimu na kumtambua kwenye hii saana kila kukicha jina langu mdomoni mwake kwa kashfa zisizoeleweka”. Alisisitiza Vanessa Mdee
eatv.tv