-->

Joslin Atoboa Sababu ya ‘Bifu’ Lake na Mr Blue

Rapa na muimbaji wa muziki wa bongo fleva Joslin ambaye aliwahi kutamba na ngoma kibao kali amefunguka na kusema yeye na rapa Mr Blue walizidiana uwezo kimuziki

Joslin akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, amesema hajawahi kuwa na bifu na Mr Blue ila anachojua yeye ni kwamba walizidiana uwezo kwenye muziki kiasi cha wadau, mashabiki kuanza kuwafananisha.

“Mimi sijawahi kuwa na tofauti na Mr Blue na wala hatukuwahi kuwa na bifu yoyote ile sema najua mimi na Blue tulizidiana uwezo hivyo kulikuwa na mchezo wa uwezo tu kati yangu na yeye, sema wadau na mashabiki ndiyo walianza kutufananisha na kutupambanisha kwa sababu walikuwa wanaona kama tuna flow na midondoko inayofanana hivi” alisema Joslin

Mbali na hilo Joslin anasema wakati bado hajatoka kimuziki alikuwa akikutana na Mr Blue na kwamba Blue alishawahi kumtabiria kufanya vizuri pindi atakapotoka kimuziki kutokana na uwezo wake.

“Kabla sijatoka kimuziki nilikuwa nakutana sana na Mr Blue na alishawahi niambia, niga siku ukija kutoka wewe watu watapagawa sana” alisema Joslin

eatv.tv

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364