-->

Bongo Movies Wafungua Tawi la Yanga

MASTAA wa Bongo Movies wanaoshabikia Timu ya Yanga wamefungua tawi rasmi kwa ajili ya kuisapoti hiyo ya Jangwani.

MIKE

Mike Sangu akiwa na Esha Buheti

Yanga imekuwa na mashabiki wengi kila kona hapa nchini na Bongo Movies wameanzisha tawi hilo ili kuwa karibu zaidi na timu hiyo.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa tawi hilo, Mike Sangu, baada ya kuona wanajitosheleza kufungua tawi lao waliamua kukutana na kuhimizana kufungua tawi pamoja na kuchagua viongozi mbalimbali.

“Tulipokubaliana tuliongea na Jerry Muro (ofisa habari wa Yanga) ambaye alitusaidia kupata usajili na sasa tunatambulika rasmi,” alisema Mike.

Aliwataja wasanii wengine wanaounda tawi hilo ambao wote ni wachezaji filamu kuwa ni, Wema Sepetu, Baby Madaha, Isabela Mpanda, Miriam Jolwa ‘Kabula’, Halima Yahaya ‘Davina’, Esha Buheti, Flora Mvungi, Jimmy Mafufu, Jack Pentizel, Mayasa Mrisho, Catherine Ambakisye ‘Mama Rolaa’, Sauda Mwilima, Hassan Moshi, Sabrina Rupia ‘Cathy’, Mary Mawigi, Vincent Kigosi ‘Ray’ na wengine wengi.

Chanzo: GPL

NUNUA FILAMU KUTOKA STEPS ENTERTAINMENT: TUNAKUFIKISHIA POPOTE PALE ULIPO:

Piga namba hizi: 0673 348 364 au 0754 256 489.

KAMA UNATAKA KUWA WAKALA WA KUSAMBAZA FILAMU POPOTE PALE:

Piga namba hizi: 0673 348 364 au 0754 256 489.

Filamu Zilizotoka Hivi Sasa >>>>HIZI HAPA

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364