-->

Cathy Awaka Kukimbiwa na Mume

MWANAMAMA kutoka katika kiwanda cha filamu Bongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’ amewatemea cheche wanaomsengenya kuwa amekimbiwa na mumewe hivyo kuwataka wamuache kwani hawezi kuachwa kamwe.

Sabrina Rupia ‘Cathy’

Sabrina Rupia ‘Cathy’

Akizungumza na GPL, Cathy alisema tangu mumewe ahamie kikazi Zanzibar maneno yamekuwa mengi sana kutoka kwa watu wake wa karibu kwamba ameachwa kitu ambacho siyo kweli kwani wako vizuri na mambo yao ya kifamilia yanakwenda vizuri.

“Nawashangaa sana wanaonisengenya kwamba nimeachwa, jamani siwezi kuachwa na mume wangu kamwe ila tumekuwa mbali kwa sababu tu ya kazi maana alihamishiwa Zanzibar na mimi nikabaki huku Dar ili kuendeleza miradi yetu mingine maana tungehamia wote huko tungepoteza vitu vyetu vingi vya maendeleo,” alisema Cathy bila kuwataja majina ‘wabaya’ wake.

Chanzo: GPL

NUNUA FILAMU KUTOKA STEPS ENTERTAINMENT: TUNAKUFIKISHIA POPOTE PALE ULIPO:

Piga namba hizi: 0673 348 364 au 0754 256 489.

KAMA UNATAKA KUWA WAKALA WA KUSAMBAZA FILAMU POPOTE PALE:

Piga namba hizi: 0673 348 364 au 0754 256 489.

Filamu Zilizotoka Hivi Sasa >>>>HIZI HAPA

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364