-->

Davina: Magufuli Ametunyoosha!

MTOTO mzuri Bongo Movies, Halima Yahaya ‘Davina’, ameweka ‘plain’ kuwa uongozi wa Rais Dk. John Pombe Magufuli si wa mchezomchezo kwani ili uweze kuishi, lazima utoke jasho kwelikweli tofauti na zamani ambapo mtu ulikuwa unaweza kupiga ujanjaujanja na maisha yakaenda.

Davina alifunguka hayo alipokuwa akitoa tathimini yake kuhusu hali ya kiuchumi alipokutana na mwanahabari wetu hivi karibuni ambapo alisema ili kuendana na kasi ya rais, inabidi wasanii wapambane kuwa na mianya mingine ya kibiashara kuliko kutegemea sanaa pekee.

“Kwa hali ya sasa hivi mtu akitegemea kazi ya sanaa peke yake itakuwa imekula kwake kwa sababu sanaa ya sasa hivi ili upate hela lazima ushurubike hasa. Hiki siyo kile kipindi cha kuishi mjini kwa kuungaunga tu halafu maisha yanaenda,” alisema Davina.

Davina

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364