-->

Flora Mbasha Akataa Hadi Jina

Msanii wa nyimbo za injili Flora Mbasha amesema swala la mahusiano na mapenzi ni ya watu wawili hivyo hataki kuweka wazi juu ya ishu yake ya kudai talaka.

Madam Flora

Akiongea kupitia eNEWZ Flora ambaye amesema anataka kuitwa madam Flora kwa sasa kwa kuwa maisha yake anayoyaishi kwa sasa yana amani na furaha hivyo anapendelea kuishi vile apendavyo yeye na kwa sasa hapendi kuongelea kwenye media kwa kuwa maisha yake hayatawanufaisha chochote.

Hata hivyo Madam Flora amesema kwa sasa hajali watu wanayoyaongea juu ya maisha yake na Mbasha kwa kuwa wengi wanaoongea hawamfahamu na wala hawajawahi hata kumshika mkono lakini pia hakusita kumuombea Mbasha kuwa Mungu ampiganie.

eatv.tv

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364