-->

Mastaa: Magufuli Ametuua kwa Njaa

Baby Madaha

Baby Madaha

Jambo limezua jambo! Kufuatia tumbuatumbua inayoendeshwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa vigogo waliokuwa wanawapa jeuri mastaa wa kike mjini, wenyewe wameibuka na kusema kiongozi huyo ‘amewaua’ kwa njaa.

Chanzo makini kililiambia gazeti hili kuwa mastaa wengi wa kike wanalalamika njaa na ndiyo maana tangu alipoingia madarakani Rais Magufuli na kuanza kuwaondoa mafisadi, wasanii hao wamekuwa hawaonekani viwanja kama zamani kwa sababu hawana mkwanja.

“Yaani wasanii wa kike wana hali mbaya sana ndiyo maana hamuoni wakiwa na mbwembwe kama zamani wamekuwa wakijifungia ndani tu hawataki kuonana na watu kwani hata hela za kwenda saluni kujiremba hamna maana wanasema waliokuwa wakiwapa jeuri wengi wao wamekumbwa na tumbua majipu,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kupata ubuyu huo, paparazi wetu aliwatafuta baadhi ya mastaa ambapo walikuwa na haya ya kusema;

ISABELA MPANDA

“Kweli tumeathirika sana na hii tumbua majipu maana waliokuwa wakitupa fedha nyingi hata ukiomba milioni wanatoa kwa sasa wanaogopa hata ukiwapigia simu hawapokei huku wengine wakiwa ni wale vigogo waliokamatwa, Rais Magufuli ametunyoosha.”

BABY MADAHA

“Kiukweli lazima iathiri kwa sababu ilikuwa rahisi kwa mtu kudhamini hata katika muvi. Kipindi cha Kikwete (Jakaya, Rais wa awamu ya nne) mtu anakupa milioni 20 au 30 kwenye muvi lakini sasa hivi, thubutu.”

MIRIAMU JOLWA ‘JINI KABULA’

“Mimi sina kawaida ya kutoka na mapedeshee, bwana’ngu ni wa kawaida sana kwa hiyo sijui kama imeathiri vipi hiyo tumbua majipu.”

Chanzo: GPL

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364