-->

Ndoa ya Lulu, Dj Majizo Yanukia

BAADA ya kuwa kimya kwa muda mrefu, staa wa filamu mwenye vituko vingi, Elizabeth Michael ‘Lulu’, ameibuka na kuweka wazi kwamba yupo mbioni kukamilisha maandalizi ya ndoa yake na mmiliki wa Redio EFM, Francis Shiza ‘Dj Majizo’.

Lulu Akiwa na Majizo

Lulu, ambaye hivi karibuni alidaiwa kuachana na mpenzi wake huyo wa muda mrefu, aliliambia MTANZANIA kwamba taarifa hizo hazikumuumiza, ndiyo maana aliamua kuwa kimya, huku akiendelea na mipango yake ya ndoa na mpenzi wake huyo.

“Siku zinakaribia na karibu tarehe ya ndoa yangu itatangazwa kwa uwezo wa Mungu, hapo ndipo waliotamani tuachane wataziba midomo, maana natarajiwa kuwa mke halali hivi karibuni,’’ aliongea kwa madoido Lulu.

Lulu aliongeza kwamba, atakapoolewa amepanga kuwa mke mwema kama anavyoishi sasa kwenye hatua za uchumba.

Chanzo: mtanzania.co.tz

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364