-->

Nyumba ya Profesa J Yakumbwa na Bomoabomoa

Dar es Salaam. Nyumba za kifahari zilizojengwa pembezoni mwa Barabara ya Morogoro kuanzia maeneo ya Kimara mpaka Kiluvya jijini Dar es Salaam zimekumbwa na bomoabomoa ya aina yake.

Pengine hilo linafahamika na wengi, lakini bomoabomoa hiyo haikumuacha salama Mbunge wa Mikumi (Chadema), Joseph Haule ‘Profesa J’.

Wamiliki wengi wa nyumba hizo hawajaanza kubomoa wenyewe kama ilivyo kwa wengine walioanza kufanya hivyo kwa hiari yao ili kuokoa baadhi ya mali kabla ya kubomolewa kwa nguvu na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads).

Hali ya huzuni na simanzi imetawala kwenye maeneo ambako wananchi wamekumbwa na bomoabomoa hiyo, wengi wao wakilalamikia sheria ya mita 121.5 kila upande badala ya ile ya awali ya mita 60.

Mwananchi jana ilifika kwenye nyumba ya Profesa J na kukutana na alama ya X inayoonyesha kuwa nyumba hiyo (pichani) inatakiwa kuvunjwa.

Hivi karibuni, Tanroads ilitangaza kuwa muda wowote itaanza utekelezaji wa kubomoa nyumba zilizowekewa alama ya X katika barabara hiyo kupisha ujenzi wa barabara kubwa na kisasa.

Tayari Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limeanza kukata umeme kwenye nyumba nyingi hivyo kuwafanya baadhi ya wenye nyumba kubomoa wenyewe kwa hiari na kufungasha mizigo.

Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Stop Over, Jumanne Juma alisema yapo majengo mengi ya kifahari yaliyokumbwa na bomoabomoa hiyo na kuwaweka wamiliki wake njiapanda.

Mwananchi

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364