-->

Odama: ‘Mkwe’ Imezingatia Maoni ya Mashabiki Wagu

Staa mrembo kutoka Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama’ ametambulisha ujio wa filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la MKWE ambapo ameleza kuwa imezingatia maoni ya mashabiki zake.

mkwe93

Kupitia ukurasa wake mtandaoni, Odama ameandika haya mara baada ya kuweka picha ya kasha la filamu yake hiyo hapo juu.

Ndugu Zangu, Jamaa, Mashabiki, Team Pamoja Na Wapenzi Wa Filamu Nchini Tanzania Leo Ni Siku Maalumu Ya Kutambulisha Cover Na Poster Maalum Inayotambulisha Filamu Yangu Mpya Ya “MKWE” Iliyoandaliwa na Kampuni Ya J-FILM4LIFE Itakayotoka Rasmi Tarehe 18.04.2016. Filamu Hiyo Ni Kwa Ajili Yako Na Kutokana Na Maoni Ya Wengi Nimeiandaa Kwa Umakini Na Katika Mazingira Ambayo Kila Mwanajamii Ataifurahia Kwani Imechunguzwa Na Wahusika Maalum Na Kuhakikisha Kua Inaangaliwa Na Rika Zote Ili Kila Mmoja Atakayeipata Aweze Kupata Kitu Ambacho Roho Yake Inaridhika. Usiikose Pindi Ifikapo Kitaani Kwako. Tag Rafiki Yako Akumbuke Tarehe Hii…. Tag, Share, Repost Kwa Rafiki Zako Ujumbe Huu… Nawapenda Sana.

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364