-->

Shilole Alia Wasanii Wenzake Kumdhalilisha

Msanii wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ameonesha masikitiko yake kufuatia madai ya kudhalilishwa na baadhi ya wasanii wenzake kwa kuipa promo video ya wimbo mpya wa zilipendwa wake, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ wa Jike Shupa.

SHILOLE23

uwena Mohammed ‘Shilole’

Kwa mujibu wa Shilole, video ya wimbo huo inaonesha matukio ya kumdhalilisha ambayo inaonekana yeye alikuwa akimfanyia Nuh enzi za uhusiano wao kama vile kumpiga na kumzodoa, mambo ambayo hakuwahi kuyafanya.

“Nimesikitishwa sana na kitendo cha baadhi ya wasanii wenzangu kuiposti video hiyo kwenye mitandao mbalimbali, huko ni kunidhalilisha kwa sababu jamii ikiangalia inaweza kunitafsiri tofauti,” alisema Shilole.

Katika video hiyo, msichana anayefanana na Shilole aitwaye Zuwena aliyetumika kama video queen anaonekana akimfanyia vitimbi Nuh huku akitafsiriwa kuwa, ndivyo Shilole alivyokuwa akimfanyia jamaa huyo.

Chanzo:GPL

NUNUA FILAMU KUTOKA STEPS ENTERTAINMENT: TUNAKUFIKISHIA POPOTE PALE ULIPO:

Piga namba hizi: 0673 348 364 au 0754 256 489.

KAMA UNATAKA KUWA WAKALA WA KUSAMBAZA FILAMU POPOTE PALE:

Piga namba hizi: 0673 348 364 au 0754 256 489.

Filamu Zilizotoka Hivi Sasa >>>>HIZI HAPA

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364