-->

Watu Wanataka Kiki Kwa Jina Langu- Shilole

ZUWENA Mohamed ‘Shilole’ analalamika akidai kuwa kwa sababu yeye ni msanii nyota wa filamu na muziki kuna watu wanataki kiki kupitia jina lake hata hivyo amelitambua hilo na atakuwa makini sana kila anaposikia jambo atafikiria alijibu au lah kwani akifanya hivyo anawatangaza wanaojinufaisha na jina lake.

“Mimi ni super star kuna watu wanatumia jina langu kujinufaisha ili na wenyewe wajulikane kama wapo kwa kutumia Shishibebi, mimi sina uhusiano na Nuh amebaki kama mshikaji na mshirika wangu katika kazi tu,”alisema Shilole.

Shilole anasema hayo baada ya hivi karibuni kuibuka maneno kuwa amerudiana na mpenzi wake wa zamani Nuh Mziwanda na kujaribu kutikisa ndoa ya msanii huyo change aliyoifunga na msichana Nawal, Shilole anasema kuwa yeye ana mpenzi wake na tayari alishamweka hadharani.

Filamu Cental

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364