-->

Wema Akanusha Kurudiana na Diamond, Amwaga Sifa kwa Zari na Tiffah

Mambo mengi yametokea wiki hii kuanzia Wema Sepetu kuachana na mpenzi wake Idris Sultan hadi Miss Tanzania huyo wa mwaka 2016 kuhudhuria birthday party ya binamu wa Diamond, Romeo na kukutana na vijana wa WCB.

WEMA344kik

Kutokana na Wema kujumuika na vijana wa himaya ya WCB, kumezuka tetesi kuwa huenda ukaribu kati ya muigizaji huyo na Diamond unaweza ukawa ni zaidi ya maex wawili walioamua kuacha bifu zao zipite.

“Yaani watu wakianza tu kuongea vizuri, bifu zao zikiisha wamerudiana, maisha lazima yaendelee, mwisho wa siku hatuwezi kuwa tunakaa tunachuniana miaka yote tutakayoishi, life is too short,” Wema alimweleza Soudy Brown kupitia U Heard ya Clouds FM.

“Mimi mwenyewe najisikia hadi amani kwamba there is no beef, maisha yanaendelea, mimi sijarudiana na Diamond, mimi namrespect kama msanii, nampenda Diamond kama msanii and I love his music and I am so glad tumeweka all this behind,” aliongeza.

Kuhusu kama anampenda mtoto wa Diamond, Tiffah, Wema alisema, “Tiffah amenikosea nini katika maisha yangu? Nimchukie Tiffah si nitakuwa mwendawazimu jamani,” alisisitiza.

Kuhusu tetesi kuwa aliwahi kumuita Tiffah zombie kama Zari alivyowahi kudai lakini Wema amezikanusha, “Hayo maneno sio ya kwangu, sijawahi hata siku moja, kwanza the way I adore babies, siwezi nikamuita baby zombie hata awe vipi.”

Kuhusu Zari staa huyo alisisitiza kuwa hana bifu naye.

“Mimi sina bifu na Zari na sijawahi kuwa na bifu na mwanamke wake yeyote Nasib, kwasababu huwa naona matatizo yangu mimi na Nasib ni mimi na yeye, Zari hana makosa, katongozwa, amedetiwa, amewekwa ndani, hana makosa hata kidogo huyo mwanamke.”

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364