-->

Aunt Afungukia Kuachana na Moses Iyobo

KUFUTAIA kuwepo kwa taarifa kuwa Mwigizaji Aunt Ezekiel amempiga chini mpenzi wake Moses Iyobo, mrembo huyo ameibuka na kusema taarifa hizo hazina ukweli.

Aunt Ezekiel na Mosses Iyobo

Aunt Ezekiel na Mosses Iyobo

Akizungumza na paparazi wetu, Aunt alisema madai hayo ya kuachana na mpenzi wake huyo yanatengenezwa na watu wake wa karibu hivyo akijiridhisha, atawatumbua.

“Wanaowaza kuwa mimi na Mose tunatarajia kugombana leo au kesho wako kwenye ndoto kali sana kwa kuwa hatujawahi kuwaza wala kufikiria kuhusu kuachana kabisa, nimeshatonywa wanaoeneza umbeya huo soon nitawatumbua,” alisema Aunt.

Chanzo: GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364