Babu Tale na Kalapina watajwa kama Chid Benz Akirudia Madawa
Akizungumza na eNewz mmoja wa wahusika wa Sober House ambae hakutaka kutajwa jina lake amesema, ikitokea Chidy atarudia kutumia dawa za kulevya tena basi wasimamizi wake ambao walimpeleka pale kwa mara ya kwanza watakuwa wamehusika kutokana na wao kushindwa kumtimizia ahadi walizokuwa wamempatia.
Aidha, ameongezea kuwa mteja ni kama mtoto mdogo ukimuahidi kitu basi lazima umtimizie lakini wao kushindwa kumuona alipokuwa akiwapigia simu kuwa anaumwa inawezekana ikawa ni sababu kubwa iliyomfanya Chidy kuondoka kwa kuwa alikuwa anaona wamemsusa ama wamemtelekeza ikiwemo na ahadi waliyokuwa wamempatia ya kumpeleka Italia kwa ajili ya matibabu zaidi.
eatv.tv