-->

Bi Mwenda Aukubali Uzee

DAR ES SALAAM: Mwigizaji mkongwe wa sinema za Kibongo, Fatuma Makongoro  ‘Bi Mwenda’ sasa ameukubali uzee baada ya kusumbuliwa na miguu ambayo imempunguzia kasi ya kufanya kazi zake za sanaa.

Akizungumza na Wikienda , Bi Mwenda alisema kuwa, sasa uzee ndiyo umekamilika kwani anasumbuliwa na miguu lakini anashukuru Mungu mambo yanakwenda vizuri.

“Nilipenda kutania uzee mwisho Chalinze lakini kiukweli sasa nimeukubali kwa sababu wala sina pa kukimbilia, miguu imeshanionesha kuwa nimezeeka,” alisema Bi Mwenda.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364