-->

‘Homecoming’ na ‘Going Bongo’ ni Funzo-Rose Ndauka

Msanii wa filamu Rose Ndauka amesema kuwa filamu mpya ya Homecoming pamoja na Going Bongo ni filamu bora zaidi kuzinduliwa nchini mwaka 2016 ambapo amewataka wasanii wa Tanzania kuiga mfano.

rose ndauka67

Akizungumza na Bongo5 Jumatatu hii, Rose alisema kila msanii wa filamu aliyoangalia filamu hizo lazima alitoka na kitu.

“Mwaka umeanza kwa changamoto ya kazi, hivi karibuni kuna kazi zilizinduliwa Homecoming na Going Bongo, ni kazi kali sana,” alisema Rose.

“Mimi binafsi nimezipenda sana, ni kazi zenye ubora, hata mimi zimenipa changamoto ya kujipanga zaidi. Kwahiyo mimi napenda kuwaambia wasanii wenzangu, hizi kazi ziwe ni fundisho kwetu mwaka huu, ukiangalia kwenye ubora wa picha, sound yaani safi kabisa,”

Rose ambaye pia alizindua magazine yake ‘Rozzie Magazine’ hivi karibuni, amewataka mashabiki wake kukaa tayari kwa ujio wa filamu zake mpya zenye ubora.

Chanzo:Bongo5

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364