-->

Huddah: Sitaki Kuolewa

MWANAMITINDO maarufu nchini Kenya, Huddah Monroe, amefunguka na kusema kwamba hana mpango wa kuolewa katika maisha yake.

Huddah Monroe

Mrembo huyo ambaye hakauki mitandaoni, amekuwa akihusishwa kutoka na nyota wa soka wa timu ya Taifa ya Kenya na klabu ya Tottenham ya nchini England, Victor Wanyama, lakini amekuwa akikana taarifa hizo na sasa ametangaza kwamba hana mpango wa kuolewa kwenye maisha yake.

“Kila mtu ana mipango yake, hivyo kwa upande wangu sina mpango wowote wa kuolewa. Hata hivyo, kama itakuja kutokea nikaolewa hatakuwa mwanamume wa Nigeria.

“Maana kuna taarifa kwamba natoka na Wizkid, sikushangaa sana kwa kuwa niliwahi kuposti picha nikiwa na msanii huyo nilipokutana naye nchini Marekani, picha hizo zikaleta maneno mengi nina uhusiano naye wa kimapenzi hakuna ukweli na sitaolewa na mwanamume wa Nigeria,” alisema Huddah.

Mtanzania

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364