Mapokezi ya Zari Leo (Video)
Zari The Bosslady ametua Tanzania, leo jioni Septemba 13, akitokea nchini Afrika Kusini kwaajili ya kuzindua duka jipya la bidhaa za nguo, Danube lililopo Mlimani City jijini hapa.
Zari ametua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa bila mtoto wake mdogo Nillan kitendo ambacho kimeonyesha huwenda mrembo huyo hajafika kwa ajili ya mpenzi wake na ni kwa muda mchache.