-->

Mlela Anavyozidi Kuingiza Mkwanja Nje ya Bongo

BAADA ya mwaka jana kula shavu la ku­cheza tamthiliya nchini Kenya kwa mwaka mmoja ambalo limeisha mwezi huu, staa wa fil­amu Bongo, Yusuf Mlela amejikuta akichekelea baada ya kupata kazi ny­ingine tena.

Akipiga stori na Risasi Jumamosi, Mlela alisema ana furaha kubwa kupata kazi nyingine inayokwenda kwa jina la Nyota ambayo ni ya miezi saba watai­fanya na wasanii wa Kenya pamoja na wa Tanzania ambao ni Daud Michael ‘Duma’, Salama Salmini ‘Sandra’ na Hasheem Kambi.

“Nimefurahi sana kwa kweli maana kazi ya kwanza ndiyo nimemaliza mwezi huu sasa nimepata nyingine ambayo tut­aifanya kwa miezi saba, najiona mwenye bahati sana kwa kweli maana Kenya ninajifunza mam­bo mengi yanayohusiana na filamu, lakini pia nitatengeneza pesa zaidi kupitia kazi yangu hii,” alisema Mlela.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364