-->

MUSA Banzi: Waansishi na Waongozaji wa Filamu Hatupewi ‘Credit’

Musa Banzi anaumizwa na kitendo cha wasanii kupewa credit badala ya credit hizo kupewa waandishi wa filamu na waongozaji.

musa banzi2

Musa Banzi

 

Banzi amewahi kuandika filamu zilizowahi kufanya vizuri kama vile ‘Shumileta’, ‘Odama’ na nyingine nyingi.

Akizungumza kwenye kipindi cha E-News, kinachoruka kupitia EATV, Banzi alisema, ‘Siku hizi wasanii ndiyo wanaopewa credit kwenye movie badala ya madirector na waandishi. Watu wanatofautisha kati ya director, producer na msanii. Hata ukiangalia movie watu hawaangalii jina wala nani kaiandaa, watamsifia msanii aliyecheza utasikia Odama umefanya vizuri sana au Riyama umecheza vizuri sana,” aliongeza.

Kwa sasa mwandishi huyo anatarajia kufanya audition kwa ajili ya kuja na movie mpya ambayo itajulikana kama ‘Odama wa Dhahabu’.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364