-->

Q Chief Atoa Siri ya Wasanii Kutoacha ‘Unga’

Msanii Q Chief amefunguka na kusema kuwa baadhi ya wasanii kushindwa kuachana na matumizi ya dawa za kulevya ni kutokana na wao wenyewe kutokubaliana na hali hiyo kutokana moyoni mwao.

Q Chief pia ametoa lawama kwa baadhi ya watu ambao wamekuwa wakijifanya kuwasaidia wasanii hao kuachana na madawa wakiwa na lengo la kutaka kunufaika nao kibiashara tu na si lengo la kweli kuwasaidia kuondokana na hali hiyo.

Q Chief anasema yeye alipitia kipindi kigumu zaidi kuachana na madawa hayo na alifanikiwa na mtu ambaye alimfanikisha kuachana na madawa hayo ni kijana kutoka mtaani ambaye aliweza kumbadilisha na kufanikiwa hivyo kijana huyo alifanya kazi kubwa ambayo serikali yake ilishindwa, mawaziri walishindwa na marafiki zake ambao walikuwa wakila bata na Q Chief walishindwa.

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364