-->

Riyama Afunguka Kutomsamehe Mtu Huyu kwa Kumdhulumu Pesa

MWIGIZAJI mahiri katika tasnia ya filamu Bongo Riyama Ali amelalamikia madalali wa kazi za wasanii kwa kuwa chanzo cha dhuluma kwa wasanii wanaotengeneza filamu, huku wao wakijinufaisha na jasho lao akiongaea na FC Riyama amedai kuwa ametapeliwa kazi yake ya Kajala.

riyama81

hajui jinsi gani umepata fedha hadi kuunga unga na kutoa filamu bila ya huruma mtu anakudhulumu mimi kazi yangu Kajala hadi leo nimetapeliwa na mtu aliyeuza kwa Steps amenilipa pesa kidogo na filamu imetoka ina muda sasa,”

Msanii huyu amelalamikia mfanyabiashara maarufu kwa filamu za zaga zaga jina tunalihifadhi kuwa alichukua kazi yake kwa makubaliano kuwa anajuana na msambazaji haiwezi kukaa foleni hivyo angepata malipo yake kwa wakati lakini ameambulia kupewa fedha kidogo huku mtu huyo hapokei simu na kumtishia kuwa yeye anajulikana.

Aidha Riyama amedai kuwa Serikali na vyama vya wasanii viangalie jinsi ya kulinda maslahi ya wasanii wanaibiwa sana,kwani kumekuwa na tabia ya udalali wa filamu kwenda kwa wasambazaji ambao kazi ucheleweshaji ambao unajenga mazingira ya Rushwa.

“Nimekuwa na busara sana kwani nashangaa yeye kulipwa fedha huku filamu ikiwa kila kitu kimeandikwa mimi Riyama Ally ilikuwaje alipwe yeye bila mimi kuwepo?,”anasema Riyama Ally.

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364