-->

Thea Ataja Madhara ya Mapedeshee

STAA wa filamu nchini, Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ amefunguka kuwa hana mpango na hategemei mapedeshee  kuendesha maisha yake kwani madhara yake ni makubwa.

Akibonga na Risasi Jumamosi, Thea alisema katika maisha yake hajawahi kutegemea wanaume mapedeshee wamwendeshee maisha yake kwani kuna hasara kubwa kwa sababu mastaa wengi wa kike wanaoishi kwa kuwategemea hujikuta wakiachwa na kurudi chini kabisa hivyo ni funzo kubwa.

“Siwezi na sijawahi kutegemea mapedeshee kuendesha maisha, mastaa wa kike wengi tumewaona wakiendesha magari ya thamani, wakiishi kwenye nyumba nzuri lakini wanapoachwa wananyang’anywa kila kitu, wanafilisika wanarudi chini, mimi tangu nimetengana na Mike Sangu sijawahi kumwanika mwanaume yeyote kwamba ni mpenzi wangu,” alisema Thea.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364