-->

Video: Harmonize Amlilia Wolper Kupitia ‘Ibaki Stori’ ya Rich Mavoko

Mapenzi ni kidonda ukiwaza utakonda. Harmonize ameonyesha bado anamhitaji Jacquline Wolper kwenye himaya ya moyo wake baada ya kupigwa kibuti.

Baada ya kusambaa kwa taarifa kuwa wawili hao wamemwagana tena huku Wolper akipigilia msumari kuwa jambo hilo ni ukweli mtupu japo Harmo alikuwa akilificha, sasa muimbaji huyo ameanza kuonyesha kuwa jambo hilo ni kweli.

Harmonize ameonekana katika kipande cha video alichokiweka Wolper katika mtandao wake wa Instagram akimuimbia mpenzi wake huyo wa zamani wimbo wa ‘Ibaki Stori’ wa Rich Mavoko kama njia ya kumshawishi mrembo huyo asahau yaliyopita.

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364