-->

Watu 32 Wafariki Katika Ajali ya Basi Karatu

Ajali mbaya imetokea Karatu Arusha katika mlima Rhotia baada ya basi dogo la St Lucky ya Arusha aina ya Coaster lililokuwa limebeba wanafunzi kutumbukia kwenye korongo na kusadikiwa kusababisha vifo kwa wanafunzi kadhaa.

Basi la St Lucky ya Arusha ambalo lilikuwa limebeba wanafunzi waliokuwa wakienda kufanya mtihani wa ujirani mwema na wenzao Karatu likiwa limetumbukia kwenye Korongo.

 

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha Charles Mkumbo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema ajali hiyo imetokea baada ya basi hilo kuacha njia na kuingia katika bonde la mto Mlera ambapo maiti wamepelekwa katika Hospital ya Lutheran Karatu.

Kamanda Mkumbo amesema kuwa kati ya maiti hizo miongoni mwao wapo waalimu ni 2 dereva 1 na wanafunzi 29 ambapo wanafunzi wa kiume 11 na wasichana 18 nakufanya jumla yao kuwa maiti 32.

Mili ya baadhi ya marehemu

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364